STD VII SAYANSI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2023

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA

MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI

05 SAYANSI NA TEKNOLOJIA

Muda: Saa 1:30 Mwaka: 2023

Maelekezo

1. Karatasi hii ina sehemu A na B zenye jumla ya maswali arobaini na tano (45).

2. Jibu maswali yote.

3, Soma maelekezo yote yaliyoko katika fomu maalum ya kujibia (OMR).

4. Jaza taarifa zote zinazohitajika katika fomu ya OMR.

5. Weka kivuli katika kila tarakimu ya Namba yako ya Mtihani kwenye nafasi husika katika fomu ya OMR.

6. Weka kivuli kwenye herufi ya jibu sahihi kwa swali la 1 hadi 40 katika fomu yako ya kujibia uliyopewa. Kwa mfano, kama jibu sahihi ni A weka kivuli kama ifuatavyo:

7. Ukigundua kuwa herufi uliyowekea kivuli si jibu sahihi, futa kivuli hicho kwa umakini kwa kutumia kifutio safe kabla ya kuweka kivuli katika herufi mpya.

8. Tumia penseli ya HB to katika kujibu swali la 1 hadi 40, na kalamu ya wino wa bluu au mweusi kujibu swali la 41 hadi 45.

9. Vifaa vya mawasiliano na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha mtihani.

SEHEMU A (Alama 40)

Katika swali 1 - 40, chagua jibu sahihi kisha weka kivuli katika herufi ya jibu hit() katika fomu ya kujibia (OMR) uliyopewa.

1. Ni ogani ipi katika mwili inaathirika zaidi kutokana na unywaji wa pombe kupita kiasi?

  1. Ini
  2. Figo
  3. Mapafu
  4. Moyo
  5. Ubongo
Chagua Jibu


2. Takamwili zipi hutolewa na mapafu wakati wa kupumua?

  1. Maji na oksijeni
  2. Kabonidaioksaidi na maji
  3. Maji na chumvi
  4. Urea na maji
  5. Kabonidayoksaidi na oksijeni
Chagua Jibu


3. Ikiwa umealikwa kuwaelimisha wanakuui kuhusu ugonjwa wa vidonda vya tumbo, je, utawashauri kuepuka aina zipi za vyakula pindi wanapopatwa na ugonjwa huo?

  1. Vyakula vyenye sukari
  2. Vyakula vyenye joto
  3. Vyakula vya baridi
  4. Vyakula vilivyo na chumvi
  5. Vyakula vyenye asidi
Chagua Jibu


4. Nini umuhimu wa seli hai nyeupe ndani ya mwili wa binadamu?

  1. Kulinda mwili kutokana na vimelea vya magonjwa
  2. Kugandisha damu katika jeraha jipya
  3. Kusafirisha gesi ya oksijeni kutoka kwenye moyo
  4. Kurekebisha joto la mwilini
  5. Kuzuia vijidudu kuingia mwilini
Chagua Jibu


5. Sikio la kati lina vifupa vitatu vilivyoungana kwa mfuatano ambavyo hupokea mitetemo ya mawimbi ya sauti na kupitisha kwenda sikio la ndani. Je, upi ni mpangilio sahihi wa vifupa hivyo vitatu?

  1. Fuame, nyundo, kikuku
  2. Kikuku, fuame, nyundo
  3. Kikuku, nyundo, fuame
  4. Nyundo, fuame, kikuku
  5. Nyundo, kikuku, fuame
Chagua Jibu


6. Katika ukuaji wa mimea, mizizi hukua kuelekea ardhini. Ni kwa nini mizizi ya mimea hukua kwa mtindo huo?

  1. Kufuata hewa na maji
  2. Kufuata maji na mwanga
  3. Kufuata mwanga na madini
  4. Kufuata maji na madini
  5. Kufuata joto la wastani na hewa
Chagua Jibu


7. Umeombwa umsaidie mdogo wako wa kike kazi ya kubainisha viumbe hai na visivyo hai. Utachagua kundi lipi kuwakilisha viumbe hai?

  1. Mti, gogo la mti, kipepeo na chura
  2. Maji, mmea wa mhindi, samaki na chura
  3. Kipepeo, chura, maji na mti
  4. Samaki, mjusi, mti na kipepeo
  5. Maji, nyuki, nyasi na nzi
Chagua Jibu


8. Mwalimu aliwafundisha wanafunzi wake kuwa udongo tifutifu ni bora zaidi kwa kilimo kuliko aina nyingine ya udongo. Ni sifa ipi inayoufanya udongo huo kuwa bora zaidi kuliko aina nyingine?

  1. Una mabonge makubwa yanayozuia maji kupita
  2. Una kichanga, mfinyanzi na maozo ya viumbe hai
  3. Huruhusu maji kupita kwa urahisi zaidi
  4. Hupitisha maji kwa taratibu sana
  5. Hukauka haraka kuliko mchanga
Chagua Jibu


9. Baba yetu alitufundisha kulima kwa kubadilisha mazao kati ya jamii ya nafaka na mikunde. Unafikiri kufanya hivyo kuna faida gani?

  1. Huongeza kaboni
  2. Hurahisisha ukuaji wa mimea
  3. Hurutubisha ardhi
  4. Huzuia mmomonyoko wa udongo
  5. Huzuia magonjwa
Chagua Jibu


10. Ukiandika neno SHULE kwenye karatasi nyeupe na kuliweka mbele ya kioo bapa, ni taswira ipi itaonekana katika kioo hicho?

Chagua Jibu


11. Moto umekuwa ukitumika kupasha joto miili yetu wakati wa baridi. Ni kwa njia gani joto hilo huufikia mwili?

  1. Mzunguko
  2. Mnururisho
  3. Msafara
  4. Mpitisho
  5. Mvukizo
Chagua Jibu


12. Endapo umepewa nafasi ya kuishauri serikali kuhusu aina ya nishati itakayosaidia kuhifadhi mazingira, utashauri kutumika kwa aina gani ya nishati?

  1. Fueli
  2. Makaa ya mawe
  3. Mafuta ya dizeli
  4. Kuni
  5. Jua
Chagua Jibu


13. Fundi simu aliangusha skrubu za simu kwenye mchanga alipokuwa akipuliza uchafu uliokuwa umejaa kwenye simu. Utamshauri atumie kifaa gani kuzipata skrubu kwa muda mfupi zaidi?

  1. Hadubini
  2. Sindano
  3. Sumaku
  4. Mfagio
  5. Kurunzi
Chagua Jibu


14. Ni badiliko gani hutokea wakati wa kupika ugali kwa kutumia unga wa mahindi?

  1. Kiumbo
  2. Kimazingira
  3. Kikemikali
  4. Kimaada
  5. Kiyabisi
Chagua Jibu


15. Ni kwa njia gani harufu huweza kusambaa kutoka ndani ya nyumba kwenda nje?

  1. Osimosisi
  2. Fotosinthesisi
  3. Respiresheni
  4. Foto-osmosisi
  5. Difyusheni
Chagua Jibu


16 Sifa za badiliko la kikemikali ni tofauti na sifa za badiliko la kiumbo. Ni sifa ipi inaonesha badiliko la kikemikali?

  1. Hakuna kitu kipya kinachotokea baada ya badiliko
  2. Hakuna tofauti kati ya uzani wa awali na ule wa baada ya badiliko
  3. Joto jingi hutumika au kutolewa wakati wa badiliko
  4. Tabia ya kitu kinachotokea baada ya badiliko inafanana na kitu cha awali
  5. Kitu cha awali kinaweza kurudia kwa urahisi half yake
Chagua Jibu


17. Kapira aliweka maji na mafuta ya taa kwenye chombo kimoja. Mafuta ya taa yalielea juu ya maji. Je, ni sababu ipi ilifanya mafuta ya taa kuelea juu ya maji?

  1. Densiti ya mafuta ya taa ni ndogo kuliko densiti ya maji
  2. Kanielezi ya mafuta ya taa ni kubwa kuliko kanielezi ya maji
  3. Kani uvutano kwa maji ni kubwa kuliko kani uvutano kwa mafuta ya taa
  4. Tungamo la maji ni dogo zaidi kuliko tungamo la mafuta ya taa
  5. Tungamo la maji ni kubwa zaidi kuliko tungamo la mafuta ya taa
Chagua Jibu


18. Ni maada ipi ina kani ya mvutano kubwa zaidi kati ya molekyuli?

  1. Chuma
  2. Mbao
  3. Hewa
  4. Mvuke
  5. Maziwa
Chagua Jibu


19. Mawasiliano ni muhimu katika jamii ili kupashana habari. Kifaa kipi kinatumika kama njia ya mawasiliano ya asili?


Chagua Jibu


20. Mwalimu wa TEHAMA aliwapa wanafunzi wa Darasa la Saba zoezi la kuchapa barua kwenye tarakilishi. Programu gani itatumiwa na wanafunzi hao kuchapa barua?

  1. Jedwali
  2. Tumizi
  3. Chapishi
  4. Endeshi
  5. Andishi
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256